IJUE APPLICATION YA "TEAM VIEWER" ITAKAYOKUSAIDIA KUBADILISHANA MAFAILI, VIDEO, NYIMBO, KUONGEA, KUFANYA MIKUTANO UKIWA MBALI NA MHUSIKA NA HATA KUTATUA TATIZO LAKO LA KOMPUTA AU SIMU UKIWA MBALI NA MTAALAMU WAKO.

Na Josephat Keraryo Nyambeya .
nyambeya@yahoo.com
how to use teamviewer
Hii ni program ya komputa ambayo inafanya kazi za kushea mafaili, kuhamisha mafaili (file ssharing), mikutano ya mbali (online meetings), msaada wa kikomputa hata ukiwa mbali kati ya komputa na komputa. Program hii ya team viewer inakupa uwezo wa kuifikia komputa nyingine bila kuwa karibu na komputa hiyo, mfano unaweza kuingia kwenye omputa ya mtu aliyepo Marekani, Mwanza, Australia, Kigoma, Nairobi au sehemu yoyote ya dunia bila wewe kuwepo sehemu hiyo. Mfano unaweza kuhamishiana mafaili na mtu aliyepo Kigoma huku wew ukiwa Mtwara kwa Dangote bila usumbufu wowote, unaweza kufuta kitu chochote kwenye komputa ya mtu uliyeingia kwenye komputa yake kwa kutumia hiyo hiyo Team Viewer.

Watu wengi haswa makampuni yenye maboss wasio na utambuzi mzuri wa komputa au matawi mengi mikoani na sehemu mbalimbali za dunia huitumia program hii ya Team Viewer kuwasiliana na wataalamu wao wa IT pale wanapokumbana na matatizo.
TEAM VIEWER INAFANYAJE KAZI?

Ili program hii ya Team Viewer ifanye kazi sharti uipakue kwenye mtandao na kuiingiza kwenye komputa au simu yako. Na pia unaetaka kuwasiliana nae aiingize kwenye simu au komputa yake , na mtakapoanza kutaka kufanya kazi (mikutano ya mtandaoni, kushea mafaili, kuelezana shida na mambo yote inayoyafanya team viewer) wote mnatakiwa muwe hewani na muifungue kwa program hii , kisha mmoja atabonyeza sehemu inayomtaka aunganishe na program hii moja kwa moja itawasiliana na itakuletea namba ambazo utamtajia mwenzako aliyepo mbali na wewe kisha ataziingiza kwenye huko huko kwenye Program yake zikiingiliana tu basi kila mmoja wenu ataanza kuiona komputa au simu ya mwenzake na kila kilichomona mtaanza kushea mafaili. Kama mnataka kuongea basi mtapitia njia hizo hapo juu na mawasiliano yataenda sawa bila shida.

WAPI INAFANYA KAZI?
Program ya team viewer inafanya kazi kwenye mifumo ya ANDROID , WINDOWS, LINUX, MAC OS, BLACK BERRY, IoS na kadhalika nakadhalika.

Team viewer ilitengenezwwa na wataalamu wa mawasiiano mwaka 2005 huko nchini Ujerumani kabla haijanunuliwa na kampuni moja la Kingereza mwaka 2014.
Kwa ufupi hayo maelezo yanatosha kukupa mwanga juu ya programu hii, usisikitike kama wewe ni mpenzi wa Muvi, nyimbo, picha, video za ngono, mahubiri, kaswida, au chochote na unamjua mwenye nacho ila huwezi kumfikia au kuzipata kwa sababu ya umbali mwambie aanze kutumia team viewer, ili akutizimie hitaji la roho yako.

Post hii imeletwa kwa hisani ya www.technbraino.blogspot.com ...Usisite kuitembelea bog hiyo ili ujipatie ufahamu wa mambo ya kidunia, kiteknolojia, kitaaluma ili ukuze ubongo wako.



Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
Powered by Blogger.
© Copyright TEKNOLOJIA KWANZA Published.. Yuvinusm
Back To Top